Afrika Kusini - Wageni wanashambuliwa na mali zao zinaharibiwa DurbanWageni wanaoishi Afrika Kusini, hasa katika mji wa Durban, wanakabiliwa na changamoto zinazozidi kuongezeka, huku biashara zao zikilengwa mara kwa mara, kuporwa, na kulazimishwa kufungwa na makundi ya wenyeji.
Abedi Jean dela croix alifanya mahojiano na Asokolo Itabelo ambaye ni mkazi wa Durban, Abedi alimuuliza kama hali ikoje kiujumla kwa wageni katika jiji la Durban, Asokolo alianza kwa kufafanua zaidi.