Drc_ Mafuriko ya ziwa Tanganyika yamesababisha watu kubaki bila makaziDrc: Kufurika kwa Ziwa Tanganyika mjini Uvira katika mkoa wa Kivu Kusini, mashariki mwa Drc, kumesababisha maelfu ya nyumba kuzamishwa na maji, makumi ya maelfu ya wakazi kuyahama makazi yao, huku usafiri na shughuli za masoko katika mji huo zikizorota kwa kiasi kikubwa.
Awali Abedi Jean dela croix alifanya mahojiano na Kelvin Bwija, mratibu wa shirika la kiraia la wazalendo wakongomani SOCICO RDC, na mtafiti wa masuala ya kiusalama mashariki mwa Drc, Abedi alimuuliza kama taarifa zenyewe zikoje kiundani, Kelvin Bwija alianza kwa kuelezea.